MAJENGO YAADHIMISHA PENTEKOSTE


 Na:Alfred Lukonge


Hapo jana Jumapili ya tarehe 21/5/2018 ilikuwa ni siku ya kusheherekea Pentekoste ambapo kwa mujibu wa imani yetu ya kikristo, tunakumbuka jinsi Roho Mtakatifu alivyoanza kufanya kazi rasmi hapa Duniani kama Bwana wetu YESU Kristo alivyohaidi kuwa akiondoka atatuachia msaidizi tukiongozwa na mistari ya Biblia kutoka (MDO 2:17-21)

Akitoa neno la mahubiri kwenye kanisa la KKKT Usharika wa Majengo lililopo Kihonda Dayosisi ya Morogoro Parish Worker wa usharika huo Bi.Happy Merry amebainisha kuwa watu wa kanisa wanatumia kigezo cha Roho Mtakatifu kwa kunena kwa lugha ndivyo sivyo, kwani Roho Mtakatifu akimtokea mtu lazima kuwe na mtafsiri kwa minajili ya watu waliopo karibu kuelewa kile kitu ambacho anakinena.

 Bi.Happy Merry akitoa neo la mahubiri katika ibada hiyo.


Parish.Merry pia amebainisha kuwa   siku za hivi karibuni watu wanaanzisha makanisa na kuwaaminisha watu kuwa  wana Roho Mtakatifu kumbe roho mtaka vitu na kujinasibu kuwa watu wakienda kwao awatatoka kama walivyokuja jambo ambalo wakati mwingine sio kweli na kuishia kuwaibia watu.

Amesema kuwa kwa mkristo thabiti Roho Mtakatifu umeondolea hofu kwa kitu chochote atakachonuia kukifanya  ikiwemo kumuongoza kuomba maombi yenye mashiko pamoja na kumsimamisha kwenye njia za Mungu wa kweli tofauti na miungu mingine.

Katika ibada hiyo kulikuwa na tukio la kuwakumbusha washarika na watu mbalimbali waliochukua kadi ili kuchangia ununuzi wa vyombo vya Kwaya ya Uinjilisti ya Sayuni ,ambapo Katibu wa kamati ya uinjilisti usharikani hapo Mzee Mboya alitoa hamasa ya kwamba ni vizuri waliochukua kadi kuonana na viongozi wa kwaya wafanye marejesho yao kwa minajili ya malengo yaliyowekwa yaweze kutimia.

 Mzee Mboya akihamasisha washarika waliochukua kadi kutimiza ahadi zao.

Kwaya ya Sayuni tunawashukuru wote waliorejesha michango yao na tunaomba Mungu awabariki wale ambao awajatoa waweze kutoa kwa wakati ambapo tuliweka siku ya mwisho ya kukamilisha ahadi ni tarehe 27/5/2018.

Comments